UHALISI WA NENO'' UKWATA''
UKWATA-Ushirika wa Kikristo wa Wanafunzi Tanzania au kwa kiingereza (TSCF)
yaani '' Tanzania students christian Fellowship''
MISINGI YA IMANI YA CCT-UKWATA
(a)
Wanachuo wa ushirika wa wakikristo wa wanafunzi Tanzania
tunamkubari YESU KRISTO KUWA NI MWOKOZI NA BWANA wa watu wote
wanaomwamini
(b) Tunaamini katika utatu Mtakatifu yaani Baba.Mwana na Roho Mtakatifu.
(c) Tunaamini kuwa maandiko matakatifu yaani Biblia kuwa ni Neno la Mungu
ambalo lina misingi ya kweli iliyo ya muhimu kwa maisha na wokovu wetu na kukiri imani ya mitume
MALENGO AU MADHUMUNI YA CCT-UKWATA
(a)
Kuwasaidia wanafunzi wampokee YESU KRISTO kuwa mwokozi na Bwana
wa maisha yao na waishi kwa kufuata kukubali
kwao,wakishuhudia,wakitangaza habari njema na kutumika katika nchi yao
na ulimwengu wote
(b) Kuwaelea wanafunzi/wanachuo katika msingi wa maishaya Kiroho kwanjia ya ibada ya pamoja kujifunza Biblia na Sala
(c) Kujenga moyo kufuata tabia ya YESU KRISTO kwa wanafunzi/wanachuo katika kuwahudumia
watu wenye matatizo ya kimwili na Kiroho nchini na ulimwenguni mwote
(d)
Kuwatia moyo wanafunzi /wanachuo katika kufikiria juu ya wito wa
kulitumiikia kanisa na kukuza mwelekeo wa kanisa na jamii
(e) Kukuza maarifa katika maandiko matakatifu(Biblia) na karama za Rohoni
SIFA ZA MWANACHAMA WA CCT-UKWATA
(a)Mwanachuo anayetoka katika kanisa lililo mwanachama wa jumuiya ya Kikristo
Tanzania(CCT) ikiwa:-
(i) Atakubaliana na katiba ya CCT-UKWATA na kulipa kiingilio atapewa kadi ya
uanachama
(ii )Atalipa ADA ya mwaka,michango na kuhudhuria shughuli zinazopangwa na
wana UKWATA wenyewe kwa uaminifu
(b)
Kwa mwanachuo anayetoka katika makanisa yasiyochini ya CCT lazima
akubali na kuwa na sifa zilizotajwa hapo juu kwa utii wa Mungu.
(c )Mwana CCT-UKWATA lazima ahudhurie shughuli,vipindi vya ibada na kutii ratiba inayopangwa kwa uaminifu.
(d)
Mwana CCT-UKWATA hai lazima awe na ushuhuda unaomtambulisha YESU KRISTO
kwa ukamilifu bila kuchafua vazi lake kwa ushuhuda mbovu.
(e)
Mwana CCT-UKWATA lazima akubali kuwa ni kiungo cha UKWATA na atumike
kwa kujituma bila kulazimishwa kwa moyo wake kiutendaji.
MWANA CCT-UKWATA ATAPOTEZA UANACHAMA WAKE ENDAPO:-
(i) Atashindwa kutimiza katiba ya CCT-UKWATA na taratibu zote zilizowekwa kwa uaminifu
(ii) Atakosa ushuhuda mzuri wa kikristo,katika CCT-UKWATA,Taasisi aliyomo na katika jamii.
(iii) Mwana CCT-UKWATA Mshirikishwa atapoteza uanachama wake endapo atashindwa kutimiza katiba ya CCT-UKWATA.
KUPATA CHETI
(i) Kila mwanachama anahaki ya kupata cheti cha UKWATA kama ametimiza masharti na kuifuata katiba.
(ii) Mwanachama atakosa cheti kama atakosa sifa za uanachama kama ilivyotajwa hapo juu bila kuvunja hata moja.
(iii) Katika kutooa vyeti kila mwaka kutakuwa na mahafali moja tu ya kuwaaga wahitimu wa fani zote
ambayo itapangwa na viongozi wa tawi.
WAEBRANIA 10:25
Wala tusiache kukusanyika pamoja kama ilivyodesturi
ya wengine na kuzidi kufanya hivyo kwa kadri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.
BWANA YESU AWABARIKI .
No comments:
Post a Comment