Ibada

TATHMINI IBADA ILIYOFANYIKA BUGANDO TAREHE 18/01/2015
..ibada ilifunguliwa kwa maombi ikifuatiwa na timu ya kusifu na kuabudu ya Bugando ambayo pia ilitoa huduma ya kusifu na kuabudu.....


muongoza ibada DR. Marko Hingi

timu ya kusifu na kuabudu





....kwaya ya Bugando pia ilihudumu ikifuatiwa na waimbaji binafsi....
mwimbaji binafsi wa USCF
wanakwaya USCF Bugando

                                                        

















waimbaji binafsi-Jackie na mwenzie
...katibu wa USCF alitoa matangazo ya usharika...
katibu USCF Bugando akisoma matangazo
.....wanaUSCF Bugando walipata neema ya kulishwa neno la MUNGU na mtumish wa MUNGU Mch. Raymond kutoka Redio maarufu jijini Mwanza ijulikanayo kwa jina la Kwaneema Fm....
                           UJUMBE: Usikubali kukata tamaa au kukatishwa tamaa ya maisha.
                                             -Daudi alikatishwa tamaa na ndugu zake kuwa hawezi kumshinda                                                           Goliath, lakini aliweza kushinda,..
                                             -Yusuph pia aliuzwa na ndugu zake, alitupwa gerezani kwa kesi isiyo ya                                                   kwake, lakini hakukata tamaa na mwisho alitimiza ndoto yake..        
                         MASOMO: 1 Samwel 17, Daudi 17:17
                                              - Mengi yalisemwa ikiwemo pamoja na kutojidharau kuona hatufai                                                         mbele za Mungu aliye juu
Mch. Raymond akitoa huduma
                  
Mch Raymond akitoa huduma

...Mtumishi aliweka wakfu kamera mpya iliyonunuliwa kupitia mkono wa wanaUSCF kwa neema ya Mungu. kamera hiyo ni aina ya Fujifilm SL 300.....


....Shukurani na sadaka za kawaida zilifuata, wakati ibada ikipambwa moto na mwimbaji binafsi, pamoja na dada Asha (MD 5)...

....maombi ya wanaUSCF wote yakiongozwa na mratibu wa maombi yalifuata na mwisho ibada ilihairishwa kwa maombi na kwaya ya USCF wakamalizia....

         TAFAKARI YA LEO: JE, WEWE UNATHAMANI GANI MBELE ZA MUNGU...?..

         UJUMBE: MUNGU HAANGALII KAMA WANADAMU WAANGALIAVYO
                           MUNGU HUVIINUA VINYONGE NA KUVIFANYA KUWA NA NGUVU

         SHUKURANI ZETU : MUNGU WETU PAMOJA NA JESHI LA MBINGUNI
                                               MUONGOZA IBADA- MARKO HINGI (MD 5)
                                               MUHUBIRI- MCH.RAYMOND
                                               KWAYA YA USCF BUGANDO
                                               TIMU YA KUSIFU NA KUABUDU BUGANDO
                                               DPS 2 NA KAMATI NZIMA YA MAPAMBO
                                               VIONGOZI WA USCF BUGANDO
                                               WANAUSCF WOTE
                                               UONGOZI WA CHUO NA HOSPITAL BUGANDO
                                               WOTE WALIOHUSIKA KATIKA IBADA HIYO

                     NYOTE MBARIKIWE NA MUNGU ALIYE HAI


.....Shalom..

...USCF-Bugando (UKWATA) inayo furaha kukukaribisha katika ibada ya kumtukuza Mungu..

...mahali ni chumba cha MD1, ....

..ni jumapili ya tarehe 18 /01 /2015...

....fika bila kukosa na ubarikiwe...

 

IBADA ILIYOFANYIKIA ST.NICOLAS ANGLIKANA 13/05/2012

Jina la Bwana  libarikiwe kwani  wanaukwata tumefanyikiwa kuhudhuria ibada ambayo ilifanyikia katika kanisa la St.Nicolas Anglikana.
Tumepewa ujumbe ambao ni  KUUSHINDA  ULIMWENGU
      1Yohana5:1-12
      Yohana16:16
Mtumishi wa Mungu alisema: Watu wa siku hizi hawajui jinsi ya kuushinda ulimwengu
wanazani kuushinda ulimwengu ni kuwa tajiri (kufanyikiwa kimaisha).

Kuushinda ulimwengu ni kushinda majaribu kama jinsi mtumishi wa Mungu Ayubu kwani yeye aliushinda ulimwengu kwa jinsi ambavyo majaribu mengi yaliyo mpata lakini Ayubu aliweza kuyashinda.
 Nikiwa na Mwana (Yesu kristo) najua kuwa nina uzima  kwani hakuna kitu ambacho kitakatisha maisha yangu

Mtumishi wa Mungu pia akasema:  Watu wakiwa na Upungufu wa Kinga Mwilini (UKIMWI) ndipo unaona watu wanahangaika  kutafuta kinga,kutafuta dawa za kuongeza kinga mwilini.
          Lakini watu wakiwa na Upungufu  wa kinga Rohoni(UKIRO) hawahangaiki kutafuta kinga rohoni,kinga ya Roho ni Yesu kristo hivyo imetupasa kumtafuta Bwana Yesu.
 
MUNGU ATUSAIDIE  ILI TUWEZE KUUSHINDA ULIMWENGU
         Asiye na Yesu kristo hawezi kuushinda ulimwengu.
.



IBADA YA PAMOJA YA UKWATA ILIYOFANYIKA TAREHE 06/05/2012

 Tunammshukuru Mungu kwaajili ya uwepo wake ndani ya ibada ni mengi ambayo Mungu amesema nasi kupitia ibada iliyofanyikia Chuoni kwetu.
Amesema nasi kwanjia ya uimbaji pia mahubiri kwa njia ya neno kupitia kinywa cha mtumishi wake
       Somo ambalo Roho Mtakatifu ametufundisha ni  KANUNI NA SIFA  ZA KUWA  MFUASI WA KRISTO:1Kor 4:5,Luka 12:42,2Timotheo2:15,Isaya 41:8,Isaya 45:1
   Kanuni na sifa hizo ni 1:KUWA MTUMWA  WA  KRISTO
                                    2:KUWA WAKILI  WA KRISTO
Ukiwa na sifa hizo  utatambua  dhamana uliyo pewa na Mungu.
Mungu amekuchagua  ili umtumikie kama jinsi  Yakobo  alivyo chaguliwa kutoka katika uzao wa Ibrahimu ndani ya Taifa  la Israel(Isaya 41:8)

 Lakini pia Yesu anatuuliza swali  anasema    NI NANI  ALIYE  WAKILI  MWAMINIFU  MWENYE BUSARA AMBAYE BWANA  WAKE ATAMWEKA JUU YA UTUMISHI  WAKE WOTE AWAPE WATU POSHO KWA WAKATI WAKE?.

Kwaya ambazo ziliihudumu katika ibada ni UPENDO KWAYA kutoka K.K.K.T-BUGANDO
pia na    WANA HAUTIKISIKI CCT-UKWATA BUGANDO
              
                SHUKRANI                                                                                                                                    UONGOZI WA UKWATA UNATOA SHUKRANI ZA DHATI KWA WANAUKWATA WOTE,KWAYA ZILIZO HUDHURIA,WAGENI WAALIKWA NA WANAFUNZI WOTE  KWA USHIRIKIANO MKUBWA KATIKA KUFANIKISHA UZINDUZI ULIOFANYIKA TAREHE 01/07/2012.
             JINA LA BWANA LIBARIKIWE KWANI AMETUTENDEA MAMBO MAKUBWA SIKU YA UZINDUZI HUWEZI KUELEZEA.
     KILA MTU ALIYEHUDHURIA SIKU HIYO ALIBAKI AKIMSHANGAA MUNGU.
        ENEO LA PARKING AREA LILIJAZA WATU KUTOKA SEHEMU MBALIMBALI ZA MWANZA.


CCT-UKWATA BUGANDO CHOIR MTALIPWA NA MUNGU MAANA TABU YENU WALA SI BURE.

SHEREHE YA KUWAKARIBISHA MWAKA WA KWANZA 2012/2013
Uongozi wa ukwata unawashukuru wanaukwata kwa ushirikiano mliouonyesha katika
kufanikisha sherehe ya kuwa karibisha wanaukwata wenzetu wa mwaka wa kwanza 2012/2013
            Mungu awabariki wanaukwata wote,Kwaya ya AICT-BUGANDO,PRAYS& WORSHIP TEAM
na CCT-UKWATA BUGANDO KWAYA(WANA HAUTIKISIKI)

No comments: