SEMINA & PRAISE N WORSHIP



USCF NA TAFES BUGANDO, WANAYOFURAHA KUKUKARIBISHA/KUWAKARIBISHA KATIKA TAMASHA LA KUSIFU NA KUABUDU LIKIFUATIWA NA SEMINA.

NI KUANZIA TAREHE 1 HADI 3 MWEZI WA TANO MWAKA HUU 2015, (IJUMAA, JUMAMOSI NA JUMAPILI)  KUANZIA SAA NANE MCHANA HADI SAA KUMI NA MBILI JIONI.

MAHALI NI DARASA LA MD 1.

KICHWA CHA SEMINA NI "KUTEMBEA KATIKA KUSUDI LA MUNGU" SEMINA HIYO ITAONGOZWA NA MTUMISHI WA MUNGU JAMES MLEKWA.

TIMU YA KUSIFU NA KUABUDU, KWAYA, WAIMBAJI BINAFSI WOTE WATAHUDUMU SIKU HIZO.

HAKIKA HII SI YA KUKOSA MAANA IMEANDALIWA KWA AJILI YAKO......

JINSI GANI

MWALIMU MWAKASEGE-SOMO LA UONGOZI

INAKUHUSU WEWE.. UWE UMEOA AU BADO...


Inahuzunisha lakini kuna fundisho kuu kwetu sote.

“Nilipofika nyumbani usiku ule, mke wangu aliponitayarishia chakula, nilimshika mkono na kumwambia, Kuna kitu nataka nikwambie. Mke wangu alikaa chini na kula chakula kimya akiwa tayari kunisikiliza. Tena nikagundua macho yake yalionyesha anaumizwa. Nilishindwa hata namna ya kuanza kufumbua kinywa changu. Lakini ilibidi nimwambie ili ajue nilikuwa nikifikiri nini juu yake.

Nataka kukupa talaka. Nilianza kusema kwa utulivu. Alionekana kutokereka na maneno yangu badala yake aliniuliza kwa sauti ya upole ‘kwa nini?’ Sikumjibu swali lake. Kutojibu kulimfanya akasirike. Akatupa kijiko na akanikaripia, ‘wewe si mwanamume!’ Usiku ule, hakukuwa na maongezi kati yetu. Alikuwa akilia kwa kwikwi. Nilifahamu kwamba alitaka kujua ni nini kimetokea kwenye ndoa yetu. Lakini kwa hakika nisingeweza kumpa jibu wala sababu ya kuridhisha; alionekana si mali kitu kwangu penzi langu lilihamia kwa Jane. Sikumpenda tena mke wangu mawazo yote yalikuwa kwa Jane. Kwa kweli nilimdharau mke wangu!

Huku moyo wangu ukijua wazi kwamba nafanya kosa, niliandika talaka ambayo ilionyesha kwamba yeye (mke wangu) angepata nyumba yetu, gari na atakuwa na hisa 30% ya kampuni yetu. Aliangalia talaka ile na kuichana vipande vipande.

Mke ambaye tumeishi nami kwa miaka 10 alionekana mgeni machoni mwangu. Nilimuonea huruma kwa muda, rasilimali na nguvu alizopoteza lakini sikuweza kurudi nyuma kwa sababu Jane aliuteka moyo wangu kisawasawa. Hatimaye mke wangu alilia kwa sauti mbele yangu, jambo ambalo kwa hakika nilitarajia. Kwangu mimi kilio chake kilinipa nafuu.

Wazo la kuachana na mke wangu limenisumbua kwa majuma kadhaa na sasa limeendelea kuimarika na kuwa jambo la hakika zaidi.

Siku iliyofuata nilikuja nyumbani kwa kuchelewa sana nikakuta mke wangu akiandika jambo mezani. Sikutamani hata kula chakula alichonipikia nilikwenda moja kwa moja chumbani na usingizi ulinichukua mara moja kwa sababu nilikuwa nimechoka baada ya kula raha za kufa mtu na Jane.

Usiku nilishtuka usingizini mke wangu alikuwa bado akiandika. Sikujali kabisa nikajifunika vyema shuka na kulala tena. Asubuhi yake alinikabidhi masharti ya talaka yake: hakutaka kitu chochote kutoka kwangu lakini alihitaji apate angalau mwezi mmoja wa kujiandaa kabla hajaachika. Akaomba kwamba katika kipindi hicho cha mwezi mmoja sote mimi na yeye tujitahidi kuishi maisha ya upendo au kawaida kwa kadiri itakavyowezekana. Sababu yake ilikuwa ndogo lakini muhimu: mwanetu wa kiume alikuwa akikaribia kufanya mtihani katika mwezi uliofuata kwa hiyo hakupenda mtoto aathirike kisaikolojia kwa sababu ya kuachana kwetu. Hili halikuwa tatizo kwangu, nilikubali mpango wake. Lakini alikuwa na sharti la ziada, aliniomba nikumbuke jinsi nilivyombeba siku za fungate yetu hasa siku ya harusi yetu. Akaniomba na kunisihi kwamba katika kipindi hicho cha mwezi mmoja niwe nambeba kutoka kitandani kwetu mpaka mlango wa kutokea kila asubuhi. Nilidhani anakaribia kuwa kichaa. Ili kufanya siku zetu za mwisho zisiwe na migogoro nilikubaliana na masharti yake ya ajabu.

Nilimsimulia Jane kuhusu masharti ya kuachana na mke wangu. Jane alicheka sana, aliona ni ujinga. ‘Hata akitumia ujanja wa namna gani talaka ni lazima’, alisema Jane tena kwa dharau. Mimi na mke wangu hatukuwahi kugusana tangu nilipomweleza dhamira ya kumtaliki. Kwa hiyo nilipombeba kwa mara ya kwanza sote tulinuniana. Mwanetu alifurahi sana na kupiga makofi nyuma yetu, ‘aah baba kambeba mama mikononi mwake’. Maneno yake yalinichoma moyoni moja kwa moja. Kutoka chumbani kwetu hadi sebuleni, halafu tena mpaka mlangoni, ni zaidi ya mita kumi nimembeba mke wangu. Alifumba macho na kusema kwa sauti laini na ya upole; usimwambie mwanetu juu ya talaka. Nilikubali kwa kichwa, ingawa nilijisikia vibaya. Nilimuweka chini nje ya nyumba.

Alienda kituoni kusubiri basi la kazini kwake nami nikaendesha gari kwenda ofisini kwangu. Siku ya pili, zoezi lilikuwa rahisi kwetu sote. Aliegemea kifuani pangu. Nilisikia harufu nzuri ya uturi aliofukiza kwenye blauzi yake. Nikagundua kwamba sijamuangalia kwa makini mke wangu kwa kipindi kirefu sana. Nikagundua hakuwa binti tena. Kulikuwa na mikunjo usoni na nywele zake zilianza kuwa nyeupe! Ndoa yetu imekula urembo wake. Kwa dakika moja nikafikiri kwa nini namfanyia hivi.

Siku ya nne nilipombeba hisia za mapenzi kati yetu zilirejea. Huyu ni mwanamke aliyejitoa kuishi nami na tumeishi kwa miaka kumi sasa. Siku ya tano na ya sita ilikuwa wazi kwamba mapenzi yetu yalikuwa yakimea upya. Sikumwambia Jane kuhusu jambo hili. Kadiri mwezi ulivyokaribia kwisha niliona raha kumbeba mke wangu na zoezi likawa rahisi zaidi. Pengine kufanya kazi hii kila siku kuliniimarisha zaidi.

Alikuwa akichagua nini cha kuvaa asubuhi. Alichagua mavazi kadhaa hakupata linalomfaa. Kisha akaguna, ‘nguo zangu zote zimekuwa kubwa’. Nikagundua kwamba mke wangu amepungua sana, nadhani ndiyo maana niliweza kumbeba kirahisi. Ghafla jambo likanichoma… mke wangu ana uchungu na maumivu makuu moyoni mwake. Bila kujitambua nikamgusa kichwa chake. Mara mtoto wetu akatokeza na kusema ‘baba ni wakati wa kumbeba mama muende kazini’. Kwake kumuona baba akimbeba mama likawa ni jambo la furaha sana. Mke wangu alimuonyesha ishara mwanetu asogee karibu na akamkumbatia kwa upendo mkuu. Niligeuza uso wangu nisije nikabadili mawazo katika dakika ya mwisho. Kisha nikambeba mikononi mwangu kutoka chumbani, sebuleni halafu mpaka mlangoni. Mkono wake laini ulikuwa umeizunguka shingo yangu kwa upendo. Nilimkumbatia mwili wake; ilikuwa ni mithili ya siku ya ndoa yetu. Lakini wepesi wake ulinitia mashaka.

Siku ya mwisho nilipombeba nilipata shida hata kupiga hatua moja. Mtoto wetu alishakwenda shuleni. Nilimshika kwa karibu na kumwambia sikubaini kwamba maisha yetu yalikosa upendo. Nikaenda zangu ofisini…. Nikashuka garini hata bila kufunga mlango. Maana nilihisi nikichelewa tu ninaweza kubadili nilichoamua…. nikapand ngazi. Jane alifungua mlango nikamwambia, ‘Samahani, Jane, sihitaji tena kumtaliki mke wangu’. Akaniangalia kwa kustaajabu, halafu akagusa kichwa changu. Akaniuliza ‘Unaumwa?’ Nikaondoa mkono wake kichwani kwangu. ‘Samahani, Jane, nimesema sitaki kumtaliki mke wangu. Nadhani ndoa yangu haikuwa na furaha kwa sababu sikuthamini undani wa maisha yetu, mimi na mke wangu, si kwamba hatupendani. Nimetambua hilo tangu nilipombeba siku ya ndoa yetu nilitakiwa kumbeba siku zote za maisha yetu, nampenda mke wangu sitamuacha mpaka kifo kitakapotutenganisha.’

Ikawa kama Jane alizinduka usingizini. Akanizaba kibao cha nguvu, akajiegemeza mlangoni na kuanza kulia. Nikashuka ngazi na kuondoka zangu. Nikaingia kwenye duka la maua nikaagiza maua mengi mazuri kwa ajili ya mke wangu. Muuzaji akaniuliza aandike nini kwenye kadi. Nikatabasamu na kuandika “Nitakubeba kila asubuhi mke wangu mpaka kifo kitakapotutenganisha”. Jioni ile nilifika nyumbani na maua mikononi mwangu, tabasamu kubwa usoni nikakimbia mpaka chumbani, nikapokelewa na maiti ya mke wangu kitandani.

Kumbe mke wangu alikuwa akisumbuliwa na saratani kwa miezi kadhaa nami nilishindwa kubaini kwa sababu nilihamishia akili yangu kwa Jane. Alijua kwamba angekufa karibuni na alitaka asiniingize katika chuki na mwanetu kama ningelazimisha talaka mapema.

Angalau machoni mwa mwanangu naonekana ni mume mwema….

Jamani vitu vidogo vidogo vizuri ni vya msingi sana katika mahusiano yetu… Siyo majumba au magari au fedha zilizoko kwenye benki. Hivi vitakupa tu mazingira ya kufurahi lakini vyenyewe siyo furaha. Kwa hiyo jitahidi kuwa na muda mzuri na mazingira rafiki ya kuwa na mwenzi wako, kuwa rafiki wa mwenzi wako. Fanya vitu mlivyofanya wakati wa uchumba na wa ndoa yenue ambavyo vitawaweka karibu siku zote. Muwe na ndoa yenye furaha. Mara nyingi watu hushindwa katika ndoa kwa kutotambua ni kwa kiasi gani walikuwa karibu wakati wa kujenga uhusiano wao

Mungu awabariki nyote mliosoma na kujifunza hapa.

....NB;, IMENAKILIWA SEHEMU...

MH. RAISI J.K KIKWETE AZUNGUMZIA KUHUSU MAHAKAMA YA KADHI...



Rais Jakaya Kikwete akifungua mkutano wa viongozi wa Kamati ya Amani Mkoa wa Dar es Salaam uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam jana. (Picha na Freddy Maro).
Rais Jakaya Kikwete akifungua mkutano wa viongozi wa kamati ya Amani mkoa wa Dar es Salaam uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kitaifa wa Julius Nyerere (JNICC) Dar es Salaam juzi

RAIS Jakaya Kikwete amefafanua msimamo wa Serikali katika mjadala unaoendelea wa Mahakama ya Kadhi, na kuweka wazi kuwa Serikali haina mpango wa kuianzisha, wala kuiendesha.

Mbali na hiyo, Rais Kikwete ambaye jana alizungumza na Kamati ya Amani ya Viongozi wa Dini mkoani Dar es Salaam, pia alielezea kusikitishwa kwake na tamko la Jukwaa la Wakristo Tanzania, lililowaelekeza waumini wao kupigia Katiba Inayopendekezwa kura ya Hapana.

Akifafanua suala la Mahakama ya Kadhi, Rais Kikwete alisema Serikali ina msimamo wa mambo mawili katika mahakama hiyo.

Kwanza, alisema Serikali haina mpango wa kuianzisha na kuiweka katika Katiba na pili, haihusiki kuiendesha na badala yake, Waislamu wenyewe ndio watakaoiendesha.

Alisema kimsingi, mahakama hiyo ilikuwepo kabla ya Uhuru na kinachotakiwa kuzungumzwa ndani ya Bunge, ni Sheria ya Kutambua Uamuzi Unaofanywa na Kadhi.

Alifafanua zaidi kuwa Mahakama hiyo ya Kadhi, haihusiki na mambo ya jinai, isipokuwa mambo ya kijamii ikiwemo talaka, mirathi na mengine ya aina hiyo.

Alitoa mfano wa Sheria ya Kiislamu, iliyokuwepo tangu zamani, ambayo inatambua chombo hicho na kusisitiza kuwa kinazungumzwa, ni uamuzi unaofanywa na Kadhi utambulike tu.

Katika mfano huo, alisema Muislamu ukigombana na mke wake, kuna mabaraza ya usuluhishi ambayo huyo mwanamke atapaswa kwenda, ila wakishindwa na ataomba talaka ambayo inaidhinishwa na Kadhi, ambaye ndiye msajili wa vyeti vya ndoa kwa Waislmau.

Baada ya kutoa ufafanuzi huo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Shehe Alhad Musa, alimshukuru Rais Kikwete kwa ufafanuzi alioutoa na kusema Wakristo na Waislamu siku zote ni wamoja na wataendelea kuishi kwa amani, furaha na ushirikiano.

Katika hilo, Shehe Alhad alinukuu Biblia katika Kitabu cha Mathayo tano, mstari wa 25, ambao unasema; “Patana na mshitaki wako, mngali njiani, asije akakupeleka kwa Kadhi na Kadhi akakukabidhi kwa Polisi na Polisi akakutupa korokoroni.”

Katiba Pendekezwa

Akizungumzia Katiba Inayopendekezwa, ambayo inasubiri kupigiwa kura na wananchi, Rais Kikwete alisema Katiba hiyo imewakilisha vitu vingi kuliko Katiba iliyopo.

Alifafanua kwamba Katiba Inayopendekezwa, imeweka haki za makundi mbalimbali ya jamii, kuliko iliyopo na kuongeza kuwa yeye binafsi ameisoma na kurudia kuisoma, lakini hajaona mahali popote ambapo ina kasoro.

Alisema isingekuwa rahisi kuweka maoni ya kila mtu katika Katiba, na kufafanua kuwa yale ambayo hayajawekwa sasa hivi, utafika wakati wake na yatawekwa.

Alibainisha kuwa haikuwa rahisi kwa maoni ya kila mtu kuingia katika Katiba Inayopendekezwa, kwani hata CCM ilikuwa na mambo 60 waliyopendekeza, lakini kati ya hayo ni 12 tu yaliyoingia.

Rais Kikwete alisema Katiba sio Msahafu au Kurani, ambayo haiwezekani kubadilishwa hata nukta. Alitoa mfano wa Zanzibar, kwamba wakati kuunda Muungano, yapo mambo yalionekana ni muhimu kubakia katika Muungano, lakini kadri muda ulivyokwenda yameondoka.

Jukwaa la Wakristo

Akizungumzia tamko la Jukwaa la Wakristo Tanzania, Rais Kikwete alisema amehuzunishwa na kufadhaishwa na tamko hilo la viongozi wa dini la kutaka waumini wao wajiandikishe kwa wingi, lakini wapige kura ya Hapana kwa Katiba Inayopendekezwa.

Tamko hilo lilitolewa na jukwaa hilo linaloundwa na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) na Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (CPCT).

Rais Kikwete alisema, tamko hilo litakuwa pia limekwaza waumini, kwa kuwawekea mipaka ya kidemokrasia na kukwaza hata viongozi wenyewe.

Alitoa mfano kwamba kwa tamko hilo, muumini hataweza kusimama na kumwambia kiongozi wa dini asiwaingilie katika uamuzi, kwa kuwa kupiga kura ni haki ya kikatiba ya kila mtu, na ikitokea hivyo, hata kiongozi husika atakwazika.

Subira kwa NEC

Kuhusu uwezekano wa Kura ya Maoni kufanyika Aprili 30 kama ilivyotangazwa na Serikali, huku kazi ya kuandikisha wapigakura ikiendelea kusuasua, Rais Kikwete alisema Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), inayoratibu uandikishaji wa wapigakura, itazungumza kuhusu walipofikia wakati muafaka ukifika.

Amani Kuhusu amani ya nchi, Rais Kikwete alisema viongozi wa dini pia wa jukumu kubwa la kuimarisha amani ya nchi.

Katika utekelezaji wa jukumu hilo, Rais Kikwete aliwataka viongozi hao wajaribu kuepuka kutumiwa na watu wenye nia mbaya, kwa sababu wanafahamu kuwa viongozi wa dini wana ushawishi katika jamii na wana watu wengi nyuma yao.

Alisema machafuko yatakayotokana na mvurugano wa kidini, hakuna mtu atakayeweza kuyazuia, hivyo ni vyema viongozi hao waendeleze mshikamano.

Alitoa mwito kwa mikoa mingine nchini, kuunda kamati za amani kama ilivyo Kamati ya Amani ya Viongozi wa Dini mkoani Dar es Salaam.

Kadhi yuko Kibiblia

Akitoa neno la shukrani, Makamu wa Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Askofu Valentino Mokiwa wa Kanisa Anglikana Tanzania, alielezea kufurahishwa na maelezo ya kina yaliyotolewa na Rais Kikwete.

Alisema pia alifurahishwa na maneno aliyonukuu Shehe Alhad kutoka Mathayo 5:25 yaliyoonesha kwamba kumbe Mahakama ya Kadhi ni ya Wakristo, maana ipo katika Biblia, na kufanya ukumbi uvunjike kwa kicheko.

CHANZO: HABARI LEO
..IMENUKURIWA KUTOKA GOSPEL KITAA BLOG

...HAPPY EASTER

......USCF BUGANDO inayofuraha kuwatakieni watu wote HERI NA FANAKA katika msimu huu wa PASAKA...

.....tamani sana BWANA YESU afufuke upya ndani ya maisha yako na ufanyike kiumbe kipya....

............tusherekehe sikukuu hii kwa AMANI, UPENDO NA FURAHA sisi na familia zetu na jirani zetu....

         1 PETRO 1; 18- 23
          ZABURI 22; 1- 11
          WAEBRANIA 10; 19- 23
           MARKO 16; 1-8.......






                                                    BE BLESSED!!!.....

WAKATI TUNAELEKEA PASAKA, BASI TAFAKARI NA HAYA....

KUHUSU KUSIFU NA KUABUDU-Sehemu ya 1


Naamini uko poa na unaendelea vizuri!!
Naamini bado una akili timamu na unajielewa zaidi una hofu ya Mungu ndani yako (Kama sivyo basi hapa kwako ni pagumu)
"KUSIFU" na "KUABUDU" ni ibaada kamili mbele za Mungu,msingi wa ibaada zote na inayopaswa kufanywa kwa makini,ustadi na furaha tele kwa ajili ya Mungu na Ibaada hiyo inawapasa wanyofu wa mioyo!!
KUSIFU-Ni ibaada ya kushukuru,kushangilia, kumkubali,kumsifia,kumwadhimisha,na kumtukuza Mungu kwa matendo yake makuu aliyo,anayo na tunayoamini anaendelea kututendea.
Unaweza kumfanyia sifa kwa yale aliyoyatenda kwa wengine au hata ujumla wa matendo yake maishani mwetu!
*Mara nyingi imetafasirika kuwa sifa ni nyimbo za haraka na shangwe Ila natamani Mjue sifa zaidi ni maudhui na makusudi ya moyo wa mtaa sifa!!
KUABUDU-Ni ibaada ya unyenyekevu,heshima na adhama. Kwa Mungu kukubali,kutii na kumuadhimisha kwa sifa na tabia zake...Hapa haijalishi amefanya chochote kwako au hajajibu maombi yako kama uonavyo Ila anaabudiwa kwa JINSI ALIVYO!
Niweke msisitizo hapa yaani hata kama Huna kazi,umefeli au umeachika bado Yeye ni Mungu tu na Ni mtakatifu tu na Ni mwema tu!!!
*Pia kwa wengi imetafasirika kuwa kuabudu ni nyimbo za taratibu,za kulia na hisia kali...lakini Nataka Mjue kuwa kuabudu ni Maudhui na mwelekeo wa Moyo!!
Sasa Nani ni mwabudu halisi na Anayemsifu Mungu kweli???
Na imempasa nini mtu huyooo....??

KUHUSU KUSIFU NA KUABUDU-Sehemu ya 2



Shalom!
..Nani mwabudu Mungu wa Kweli na imempasa kufanyaje???
LEO
Natamani kusisitiza mambo makubwa mawili tu katika sifa na kuabudu!!
Yaani haya yakae moyoni na kichwani mwa yeyote anayetamani kuugusa moyo wa Mungu kwa sifa na kuabudu,nayo ni haya;
1.LAZIMA KUMJUA NA KUMFAHAMU SANA HUYO MUNGU NA KUWA NA UHUSIANO NAYE.
Huwezi kufanya ibaada yeyote kwa Mungu ikawa ya maana kama unamsikia tu na humfahamu kabisa....imetupasa kumjua tena kumjua zaidi,tena kuwa na uhusiano naye wa karibu....maana kwa Kadri unavyomjua zaidi ndivyo unazidi kumpenda yeye na Kumsifu na kumuabudu kweli!....na hapo Ndio maandiko yanasema "Kusifu kwawapasa wanyofu wa mioyo"...Okey ngoja nitoe mfano huu,Kumsifu Mungu wakati hata hamna uhusiano wa karibu na sawa na kuona mjini gari aina ya Hammer ambayo iko mitaani kwenu na ukaanza kuwasimulia wenzio..."Oyaaa unaona ile hammer,yaani nyumba yetu hii unapita mtaa mmoja ndio nyumba ya mwenye gari ile aisee,yaani ile gari kali kishenzi yaani duh,Nyie Acheni tu mtaa wetu mambo Safi hahaha" sasa hapo wakikuuliza ni Tsh ngapi au umewahi kupanda au anakufahamu unabaki tu Aaah mmmm Oooh...Acha bwana hilo sio lenu, jivunie chenu...JIVUNIE MUNGU MAISHANI MWAKO,SIO KUMSIKIA TU!!
2.LAZIMA MUNGU PEKE YAKE NDIO AINUKE(AWE MAARUFU)
Yaani katika sifa na kuabudu usijitahidi kujiinua au kutaka kuonekana wewe au timu yenu au mchungaji wenu au Kanisa lenu Ila Mungu pekee Ndio wakuinuliwa!!
Kuna ukuta mwembamba sana kati ya kutafuta sifa na umaarufu au kujiona na unyenyekevu wa kutaka Mungu pekee Ndio aonekane!!
Tena sio kwa maigizo bali toka moyoni... Na ukiwa na moyo wa unyenyekevu utashangaa una Amani tele hata uende wapi au watu wawe kumi tu au vyombo visiwepo au sare zisiwepo hata usipopewa maji au nauli na popote ulipo kwa kuwa umeamua kumfanyia Mungu ibaada basi utashangaa sana udhihirisho wa nguvu za Mungu!!!
Tabia za kuonyeshana na watu ufundi wa Sauti au kucheza na kusahau kuwa malengo ni kumuabudu Bwana basi hapo ibaada yote huwa sifuri maana tumejitwalia utukufu machoni pa watu.
(Ila pia haimanishi pia kuwa sifa na kuabudu vinapaswa kufanyika ovyoovyo..ustadi unahitajika mno)
Mungu awasaidie sana wote mnaokaa mbele kuwaelekeza watu au kuwaongoza uweponi mwake ili Mjue hamfanyi kwa ajili yenu Ila.kwa ajili ya Mungu!!!
.....Je ladha ya Kusifu na kuabudu inatokana na.viungo gani???

KUHUSU KUSIFU NA KUABUDU-Sehemu ya 3


Shalom ndugu yangu!
Naamini unaendelea vema na maisha yako na ninambariki Mungu sana kwa ajili yako na nimemwomba roho mtakatifu akusaidie kuendelea kuelewa somo hili!
Mara ya mwisho niliongelea mambo mawili makubwa kwanza ni Lazima Mtu anayetaka Kumsifu na.kumuabudu Mungu kweli lazima awe na uhusiano naye thabiti na pili katika sifa na kuabudu sio wewe au Kanisa au chochote kuinuliwa zaidi ya Mungu mwenyewe!
...Na nikaacha swali....JE NI VIUNGO VIPI HULETA UTAMU WA KUSIFU NA KUABUDU!!
Basi ninamshukuru sana Mungu kwa ajili yako na natamani niseme nawewe kwa habari ya uzuri wa sifa na kuabudu!
Sisi huwa tunadhani uzuri wa sifa ni Muziki(Melody),nyimbo tuzipendazo Sisi, mavazi yetu,mitetemeko ya waongoza sifa,machozi labda na mihemuko na hapo tunaweza kuruka na kucheza sana lakini hata kama Hayo yote huwepo au ni muhimu Ila msingi wa Utamu wa sifa na kuabudu ni haya yafuatayo;
1.Ibaada ya sifa na kuabudu yenye Utamu mbele za Mungu ni ile inayofanywa na Moyo wa kumpenda yeye,moyo Safi na wenye nia thabiti ya Kumsifu na Kumuabudu!!
2.Siyo nyimbo uzipendazo wewe ndio zinaleta utamu wa sifa mbele za Mungu,sio upendazo wewe maana sio kwa ajili yako Ila kwa ajili yake mwenyewe.... Ingawa ukizama sana utagundua kuwa kile roho mtakatifu anataka na wewe unaingiwa kupenda kile atakacho!!!
*Sasa natoa tahadhari tu.... Acha ubinafsi wa kutaka Kusifu na kuabudu kwa matakwa yako Ila msikilize sana roho ili mara zote umeona wingu lake!
3.Na tatu ni ile hamu ya kumtaka Mungu Atukuzike katika sifa na kuabudu ndio inafanya moyo wako uwe mnyenyekevu na kwa hakika Mungu ajidhihirishe na sio kuwa na hamu ya kutaka kusifiwa au kupongezwa baada ya uwepo kudhihihirika!
*Unajua Mungu akisifiwa hushuka lakini ile hamu yako ya kumuona Mungu zaidi na sio Kiasi wewe uonekane kama wewe ndio huwa unasifu na kuabudu mpaka uwepo unashuka!
4.Na mwisho;Ili ibaada ya Kusifu na kuabudu Iwe na tamu....Ni mara zote ikiwa unafanya ibaada ya sifa na kuabudu lazima uwepo umoja kati ya moyo wako au roho yako na nafsi yako na mwili wako lakini pia ikiwa mnafanya ibaada mkiwa wengi basi iwepo nia moja na mara zote muonekano wako, mkao wako na mavazi yako,yakupe nafasi ya kuwa na utulivu mbele za Mungu.... Haiwezekani ibaada ya sifa na kuabudu Iwe tamu wakati moyo na akili yako na nafsi yako havina ushirikiano....na huwezi kuwa huru kufanya chochote mbele za Mungu kama kucheza,kulia au kurukaruka hali mavazi yako yana thamani kuliko hiyo ibaada kiasi huwezi hata kupiga magoti,huwezi kucheza kwasababu ya hadhi au cheo chako au mavazi yako yanakubana au yanawakwaza wengine!!
Natamani roho mtakatifu akusaidie kuelewa haya,maana ibaada.ya sifa na.kuabudu ni ya Mungu mwenyewe na wakati wote kumbuka "ALITUUMBA ILI TUMUABUDU"
Basi wakati mwingine nitaendelea kuzungumzia kwa kina "Kwanini Sifa na kuabudu maishani mwetu? na nini uhusiano wake na makusudio ambayo Mungu alituumba nayo"

KUHUSU KUSIFU NA KUABUDU-Sehemu ya 4


Shalom wana wa Mungu!

Wajoli na Wajeuri wa Bwana!
Tumekuwa na mfululizo wa kupendeza kuhusu sifa na kuabudu,na tangu tumeanza leo ni sehemu ya nne kati ya tano...na leo natamani kuzungumzia "Kwanini Sifa na kuabudu maishani mwetu" yaani muunganiko wa sifa na kuabudu na hatma za maisha yetu!
*Najua wengi tunajua Kusifu na kuabudu ni sehemu ya ibaada mbalimbali makanisani na ndio maana watu huanza kwa maombi,sijui matangazo kisha Kusifu na kuabudu, neno,sadaka na mengineyo Ila leo natamani nikujuze kuwa sifa na kuabudu ni zaidi ya hapo!!
Kusifu na kuabudu ni ibaada endelevu kila siku na kila mahali na kwa kila namna!
Ile ifanyikayo kanisani ni namna ya pamoja ya Kusifu na.kuabudu kwa upamoja na kwa utaratibu tuliojiwekea na kama watu wakibaki na picha hiyo pekee hawatafanya ibaada hiyo kwa ukamilifu!!! 

ZINGATIA UKWELI HUU!!
Kila mtu ameubwa kwa kusudi maalum hapa duniani na kila mtu amepewa uwezo fulani halisi unaomwezesha kufanya mambo yale yampasayo kwa urahisi kuliko yeyote mwingine(Yaani kwa mfano mimi sijitahidi kusheresha au kuchekesha maana ipo ndani naturally) na.uwezo huo huitwa kipaji na wazungu huongea kwa maringo zaidi "Gifts & Talents".....na kwa ujumla wake woote mambo haya ili tumwabudu Mungu!
Sasa kama tuna majukumu ya kufanya na hayo yote ni kwa ajili ya Kumwabudu Mungu na kuyafanya majukumu hayo ndio kuishi kwenyewe...tunaachaje kumwabudu Mungu??
Ile hali ya kujua kuwa hakuna jambo unaloweza kufanya kwa akili yako na uwezo wako binafsi na ule ukweli kuwa yote ufanyayo ni kwa utukufu wa Mungu....itakulazimu kuabudu tu,isipokuwa kama umeamua kuwa na Kiburi cha uzima na kujiona kama umejiumba mwenyewe!!
"Katika sifa Mungu hushuka" naamini umewahi kusikia sentensi hiyo Ila unadhani ni kwa ajili ya ile sifa ya kanisani pekee...Je hujawahi kusikia wale watu wa kale waliowahi kushinda vita kwa sifa?? Popote ambapo Yesu anasifiwa lazima uwepo wake uwe Kamilifu.... Sasa ukitaka mambo yako yaende sawia na kwa Ushindi lazima ukubali tu kujumlishia na Ibaada ya sifa na kuabudu!!

Kusifu na kuabudu ni kama vile kusema....MUNGU NI WEWE PEKE YAKO,HAYA YOTE NI YAKO,SHUKRANI TUKUZO NA SIFA ZOTE NI ZAKO,UMETUPA HIVI VYOTE KWA UTUKUFU WAKO,AHSANTE JEHOVA MAANA NI WEWE!!
Yaani kwamba sio kwa uwezo wako wala akili yako bali ni kwa Neema ya Mungu tu!!
Kusifu na kuabudu ni wakati wa shida na wakati wa raha,ukiwa na kusanyiko na hata ukiwa peke yako,ukiwa nyumbani na hata ukiwa mbali,kwa mavazi,muonekano, kelele, kula,kuongea,kufanya kazi na hata katika kujifurahisha!!
Muhimu kujua kuwa Umeumbwa ili umuabudu Mungu,utafundishwa kuwa mtumishi ama kuishi hatma yako au utafunzwa kuwa na ndoto au kuacha Alama itakayodumu ni sawa kabisa lakini msingi wa yote haya ni ili Mungu atukuzike..... Watu wamjue Mungu,waupokee Ufalme wake na wamuishi yeye....na hapo Ndio tunasema Maisha ya Ibaada,na.hiyo ibaada ndio Kusifu na Kumuabudu!!
Unaweza ukachoka Kumsifu alivyo mwema maishani mwako lakini kila uonapo watu wanakufa, wengine wanaumwa na hawa wapata shida....na hayo yawapatayo wenzio wewe huyashuhudii basi choka salama....na ukimjua Mungu sawasawa kuwa yeye hata nini kitokee duniani hakibadilishi Umungu wake...na kama ukijua ni baba yako,na AHADI zake kwako ni za milele,hutaacha kumuabudu leo kwasababu una mashida na machangamoto....Ila utamwabudu tu kwa kuwa yeye ni Mungu na tumaini lako la kesho maana ni hakika na Amina!
Mungu ni mwaminifu sana mara nyingine ni kiburi tu ndio huwa kinatufanya tumsifu na kumuabudu sana aitha tukiwa tuna vingi au tukiwa hatuna basi tunamlilia, na huo kwa hakika ni utoto!!
Basi Mungu akusaidie kuwa na maisha ya Kusifu na Kuabudu kila siku, kila wakati na kila mahali bila kujali nini wala nini na hakika uwepo wa Mungu hautapungua maishani mwako!!!
Kabla ya saa ile ya Agano nitamalizia sehemu ya tano na ya mwisho kwa habari ya mambo makubwa mawili;
i. Namna ambazo unaweza kufanya ibaada ya sifa na kuabudu
ii. Mambo yakupasayo kuzingatia uwapo mstari wa mbele katika kuwaongoza wengine katika sifa na kuabudu!!
Ahsante Bwana Yesu kwa kila asomaye na kuelewa somo hili,lisaidie Kanisa lijue kina na msingi wa Ibaada kuwa ni SIFA NA KUABUDU....maana hata Malaika, maserafi, makerubi,wazee 24,wenye uhai wa nne na Sisi watakatifu tuliyo duniani na hata saa ile ya mwisho kule mbinguni biashara ni moja tu "KUMSIFU NA KUMWABUDU MUNGU"

KUHUSU KUSIFU NA KUABUDU-Sehemu ya 5(mwisho)


Shalom!
Yesu Kristo asifiwe sana!
Naamini uliyekuwa unafuatilia mfululizo huu umejifunza mengi na kubarikiwa pia,leo katika sehemu ya tano...Kuhusu kusifu na kuabudu, kama nilivyoahidi sehemu ya nne,tutaangazia mambo mawili makubwa;

I.NAMNA UNAVYOWEZA KUFANYA IBAADA YA SIFA NA KUABUDU!!
Kumfanyia Bwana ibaada,inategemeana sana na mahusiano yenu...yaani ningeweza kuwianisha na Mama na mwanae,namna ya kumlisha inategemea sana na urahisi wa mtoto huyo kula na kushiba, mwingine hula akipakatwa,mwingine hula akiwa anaoga, mwingine akiwa peke yake,muhimu ni kuwa mtoto amekula!!
Ibaada njema ni ile inayoanzia ndani ya kilindi cha moyo kabisa kwa upendo mkubwa,hivyo unaweza kufanya ibaada hiyo kwa namna nyingi,na hizi ni chache ambazo zimewahi kutumika na watumishi mbalimbali katika Biblia!
Unaweza Kumsifu na Kumwabudu Bwana:
1.Kwa kuimba,Iwe kanisani au popote pale-na hapa inaweza kuwa nyimbo za vitabuni, tenzi au zaburi au nyimbo mpya za kutoka moyoni mwako unapotafakari ukuu wa Mungu!
2.Kwa kupiga kelele-hii inaweza kuwa kelele zisizo na mpangilio au vigelege au miluzi au kelele zenye mpangilio wa nyimbo fulani!
3.Kwa kucheza -furaha ya mdundo unaoanzia ndani na sio ilimradi tu kuna muziki,na kwa habari ya kucheza unaweza kucheza hata kama hakuna muziki wowote
4.Kwa ubunifu na kazi za sanaa-mfano uchongaji,uchoraji, uigizaji na kazi nyingine za sanaa ambazo mwisho wa siku Ni Mungu ndio anasifiwa na kuabudiwa peke yake
5.Kwa kulala -unaweza ukalala namna yeyote ile kama ishara ya kujinyenyekesha mbele za Bwana
6.Kwa kupiga magoti
7.Kwa kukaa kimya mbele za Bwana
8.Kwa Kulia
9.Kwa kucheka
10.Kwa kunena kwa lugha nyingine,ziwe za duniani au lugha za kimbinguni!
11.Kwa kuomba
.....Sasa sifa na kuabudu inawiana na kuingiliana sana na maombi japo unaweza Kumsifu na Kumwabudu Bwana kwa maombi!!
Hizo ni chache katika namna nyingi,ambazo unaweza kujidhihirisha mbele za Bwana!!
Watu wengi wamechukuliwa na sifa na kuabudu ile ya kuimba na kucheza labda na kulia kanisani kwa maombi,na ni sawa tu!
Ila jambo la pili ni

II.NAMNA IMPASAVYO KUWA YEYOTE AKAAYE MBELE KUONGOZA WENGINE KATIKA IBAADA YA SIFA NA KUABUDU!
Wengi hufanya kama mazoea au utaratibu tu wa ibaada kwasababu wameshaguliwa au wamefanya mazoezi au wanajua au wana vipaji lakini ni zaidi ya hapo,imekupasa. Kuwa moyo mnyofu na Ibaada nzuri huanzia ndani yako kwanza kabla wengine hawajapotelea katika wingu,
1.Imempasa mtu huyu kuwa mtakatifu/mtauwa na anayempenda Mungu kiasi cha kupenda kumfamyia ibaada hata akiwa peke yake kabla hata kuwa mbele za watu
2.Imempasa kuwa na Neno la kutosha moyoni mwake,sio maandiko ya kukariri
3.Imempasa kuwa mwombaji, maana imempasa kusikia sauti ya Mungu wazi wazi ili awapo madhabahuni asifanye kwa mazoea
4.Imempasa kuwa na muonekano usioleta maswali kwa watu,yaani mavazi,mapambo na hata kutembea tu.
5.Imempasa kuwa na Amani na watu maana ikiwa mtu huyo ana Ugomvi au maneno maneno na watu,ibaada hiyo haiwezi kukamilika
6.Uongo,uzinzi,Umbeya, Unafiki na udhalimu wowote ule usitajwe kwake akaaye mbele za watu!...maana sifa na kuabudu kwa mwenye dhambi ni kelele mbele za Mungu!
7.Imempasa kuwa mnyenyekevu na aliye jaa hekima,na asiyejaribu kujitutumua au kujiona ni yeye na.bila yeye uwepo ule usingeshuka!
Lazima umaarufu, vyeo,elimu na hadhi viwe chini ya Utukufu wa Mungu,hivyo yeyote akaaye mbele za watu ajue kabisa kuwa yuko hapo kwa ajili ya Kumsifu na Kumuabudu Mungu tu na sio kuonekana!!
Mungu Roho mtakatifu akusaidie sote kuelewa sana zaidi ya maandishi haya,ili ibaada zetu za sifa na kuabudu, ikiwa ni za binafsi au mbele ya watu zipate kibali mbele za Mungu!
Mungu akuwezeshe na Mungu akunyenyekeshe ewe Mwabudu!!
Mpaka hapa Nimemaliza kwa habari ya Kusifu na kuabudu na ninayaacha kwako wewe kujifunza na kufundisha na kushare na wengine pia!!
*Najua utakuwa unajiuliza mbona hamna mistari ya Biblia,ndio! sitaki watu wanaokariri Nataka wanaoelewa!!!
Mungu akubariki sana wewe rafiki yangu!!
*Karibu sana katika Ulimwengu wa Kusifu na Kuabudu,kwa roho na kwa akili kwa kupenda!!

***MWISHO***
(c)King Chavvah, 2014
+255 713 883 797

MAMBO MATANO NILIYOJIFUNZA KUTOKA KWA PENSELI!!

MTENGENEZAJI WA PENSELI ANAYO MAMBO 5

NIYAPENDAYO,NA HAYO NI MAFUNZO KWA PENSELI NA SISI LEO!!!

Mtengenezaji wa PENSELI aliiambia penseli haya na mimi leo ninawaambia ninyi;

1.Eeeh PENSELI popote utakapogusa utaacha ALAMA (Haijalishi ni vizuri au vibaya)
>>>NA WEWE PIA KILA UNAPOPITA MAISHANI MWAKO UNAACHA ALAMA KWA WATU.

2.Eeeh PENSELI najua unaweza kukosea mara nyingi,basi usijali,juu yako upo MFUTO ili kufuta kila alama mbaya isiyotakiwa.
>>>NA WEWE PIA NAKUAMBIA HATA UKIFANYA MAKOSA KIASI GANI,MFUTO WA DAMU YA YESU UKO JUU YAKO.....Hakuna awezaye kurudi nyuma kuanza upya,ila pale ulipo panaweza kuwa hatua ya mwanzo mpya!

3.Eeeh PENSELI,Kitu cha muhimu sana kwako ni kile ambacho KIKO NDANI YAKO(Risasi ya graphite),Hata kama uwe na umbo ama umbile lenye mapambo kiasi gani!
>>>NA WEWE PIA TAMBUA YA KUWA KUSUDI LA KUISHI NDANI YAKO NDIO MUHIMU SANA MAISHANI MWAKO KATIKA KUMPENDEZA MUNGU,YAANI LILE MUNGU ALILOKUANDIKIA na haya mengineyo ya nje ni mbwembwe tu!

4.Eeeh PENSELI Hauwezi kuandika vizuri mpaka ukubali KUCHONGWA VIZURI ili uwe sharp(sio ombi unless unataka kuwa pambo)
>>>NA WEWE LAZIMA UJUE JAMBO MOJA KUWA ILI KWENYE MAISHA YAKO UUFURAHIE MWITO WAKO,LAZIMA UKUBALI KUCHONGWA AMA KUPITIA MAGUMU ILI UJIFUNZE KUKUA NA KUKOMAA.

5.Eeeh PENSELI pamoja na yote hayo bado huwezi kuandika au kuifurahia kazi yako,ni lazima UKUBALI KUSHIKWA NA MKONO HODARI ili mwandiko au mchoro uwe bora!
>>>NA WEWE PIA LAZIMA UKUBALI KUSHIKWA NA MUNGU MWENYEWE NA KUFUATA NENO LAKE NA KILA AKITAKACHO NA HAPO NDIO UTAPONA NA KUWA NA FURAHA MAISHANI MWAKO!!!

Ubarikiwe sana kama umenielewa na ukiweza SHARE na wenzako wasome!!!